Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mara kimelaani vitendo wanavyofanyiwa baadhi ya viongozi wa chama hicho ikiwa ni kukamatwa pasipo sababu za msingi na kuwekwa ndani pasipokuwa na dhamana yeyote huku wakibambikiziwa kesi mbalimbali.
Kauli hiyo imetolewa na baadhi ya viongozi wa chama hicho katika
kikao ilichofanyika kwenye ofisi ya (CHADEMA) Manispaa ya Musoma ili kuweza
kuangalia mstakabali wa uchaguzi wa serikali za mitaa zijazo hapo mbeleni.
Chacha Heche ni katibu wa chadema mkoa wa mara
alisema kuwa baadhi ya viongozi wakiwemo madiwani wamekamatwa na kubambikiwa
kesi ikiwa ni pamoja na kuwekewa pingamizi la kuchukua fomu za kugombea
nyadhifa za uongozi.
“Diwani
wangu wa Serengeti pamoja na watendaji wangu wamekatwa na kuwekwa ndani na
wengine wanabambikiwa kesi za meno ya Tembo ili chama changu kiweze kuanguka”
alisema Chacha.
Kwa upande
wake saguda joseph Mnawa mwenyekiti wa chadema wilaya ya Serengeti ambaye pia
ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama kanda
ya ziwa anazidi kukemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi wa serikali.
“Tunasema
hatutaogopa hatutakejeri mtu bali tunachotaka ni haki kutendeka kwa
wananchiwetu” aliseama.
Aliongeza
kuwa viongozi wa serikali ndio chanzo
kikubwa cha uchochezi wa fujo pale wanapotafuta sababu zisikuwa za msingi ili
kuweza kuwakamata viongozi wa chama pinzani waweze kupata nafasi ya kupenya
waondokane na vitendo hivyo na kuachia wananchi waweze kufanya maamuzi yao.
….Mwisho…..
No comments:
Post a Comment